TABIA ZA UPENDO WA KWELI


 TABIA ZA UPENDO WA KWELI

➖➖➖➖➖➖➖➖

1Korintho 13:4-8

4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;

5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.


KEY POINTS

➖➖➖➖➖

1.UPENDO HUVUMILIA

Ukiona unaweza kumvumilia mtu hata kama amekukosea,basi tambua kuwa unampenda,ila usipoweza,kufanya hivyo haumpendi mtu huyo


2.UPENDO HUFADHILI

Fadhili limetokana na na Fadhila..ni kama vile kumsaidia mtu ambaye hakuwa na msaada.


Unapofadhili(unapowasaidia wengine) ni tabia mojawapo ya upendo.


Ukiona husaidii wengine..wewe hauna Upendo na hauna Mungu ndani yako


3.UPENDO HAUHUSUDU

Husudu limetokana na neno Husuda,


Husuda ni hali ya wivu mbaya .

Ukiona unahusuda(kijicho) dhidi ya ndugu zako basi hauna upendo na wala hauna Mungu ndani yako


4.HAUJIVUNI

Ukitaka kila kitu uonekane wewe ndo mwamba..nenda kalale tu kazi imekushinda..huna upendo


5.HAUONI UCHUNGU

Huwezi kunambia kuwa unanipenda halafu unatunza mauchungu Moyoni hadi unaumwa..huo sio upendo


6.HAUKOSI KUWA NA ADABU

Unawezaje kujifanya unaupendo halafu ukakosa adabu?


7.Huvumilia,huamini,yote


Tupendane.maisha hapa Duniani ni mafupi sana.tuache unafiki 


Ezekia Chavala

OGS:Dir,

ogschavala@gmail.com

+255621029725

https://chat.whatsapp.com/K3lnh9YaO7Y2Z3SA2MBudI


No comments

Dr Mgasa Mhoja. Powered by Blogger.